Timothy Lugembe,
Mwanakwetusports.
Kilichoonekana kama jambo la kawaida kwenye machapisho ya mshambuliaji wa Ufaransa, Michael Olise, wakati wa Kombe la Dunia, sasa kimeibua simulizi tofauti baada ya kufahamika sababu ya picha zake zilizoonekana kuwa na ubora wa chini(low quality).
Tangu kuanza kwa kombe la Dunia, Olise amekuwa akichapisha picha zilizokuwa na ubora wa chini kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii. Hatua hiyo iliwafanya mashabiki wengi kuamini kuwa ilikuwa sehemu ya mtindo wake au ujumbe uliohusu mustakabali wake, hasa baada ya kufuta machapisho yote kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Taarifa zinaeleza kuwa mpiga picha wake binafsi alishindwa kuingia Marekani kwa ajili ya Kombe la Dunia kutokana na changamoto za VISA.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, mpiga picha huyo aliendelea kupiga picha za Olise akiwa nyumbani kupitia matangazo ya televisheni, huku Olise akiendelea kuzichapisha katika mitandao ya kijamii wakati wote wa mashindano.
0767915473,
lugembetimothy01@gmail.com

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
Post a Comment