Timothy Lugembe,
Mwanakwetusports.
Hali ya sintofahamu imezidi kuikumba klabu ya Simba SC baada ya taarifa kuibuka kwamba Kocha Mkuu wao, Fadlu Davids, yupo kwenye hatua za mwisho za kuondoka na kujiunga na moja ya timu kubwa nchini Morocco.
Taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika zinaeleza kuwa Davids amepokea ofa ya kuvutia kutoka klabu ya Morocco, ikiwa ni pamoja na mshahara mara tatu ya kile anacholipwa kwa sasa na Simba SC, Hali hiyo imeifanya Simba kukumbwa na wakati mgumu wa kumbakiza kocha huyo ambaye kwa mujibu wa vyanzo, ameshajipanga kuondoka pamoja na benchi lake lote la ufundi.
Ripoti zaidi zinaonyesha kwamba Simba tayari imeanza mchakato wa kutafuta mrithi wa mikoba ya Fadlu, huku ikijipanga kwa maisha mapya bila kocha huyo ingawa klabu hiyo imejaribu kwa jitihada kubwa kumbakiza, dalili zote zinaashiria kuwa safari yake nchini Tanzania inakaribia mwisho.
0767915473,
lugembetimothy01@gmail.com.
Post a Comment