Timothy Lugembe,
Mwanakwetusports.
Klabu ya soka ya FC Barcelona imekumbwa na pigo kuelekea kuanza kwa msimu mpya wa mashindano baada ya halmashauri ya Jiji la Barcelona kukataa kutoa lesseni kwaajili ya kuruhusu uwanja wa Spotify camp Nou kutumia kwenye michezo ya klabu hiyo.
hatua hiyo imetokana na kuchelewa kwa ukamilishaji wa baadhi ya kazi muhimu kwenye uwanja huo, zikiwemo sehemu za VIP, paa, mifumo ya umeme na ulinzi, pamoja na mazingira ya nje ya uwanja, Kutokana na hali hiyo, Barcelona haijapata kibali rasmi cha matumizi kutoka kwa halmashauri ya jiji, jambo linalowazuia kupokea mashabiki au kuandaa mechi yoyote rasmi.
Mashabiki wa Barcelona pamoja na viongozi wa klabu hiyo wameonesha masikitiko yao kutokana na hali hiyo, hasa ikizingatiwa kuwa uwanja huo ulitarajiwa kufunguliwa upya kwa heshima ya nyota wao wa zamani Lionel Messi, ambaye pia angeweza kuheshimiwa kupitia mchezo wa Gamper mwaka huu.
Kwa sasa, klabu hiyo inasubiri maamuzi ya mwisho kutoka kwa halmashauri ya jiji, huku ikilazimika kuandaa mipango mbadala kwa ajili ya michezo ya mwanzo.
0767915473.
lugembetimothy01@gmail.com.
Post a Comment